
WATU watano wamefariki dunia leo asubuhi na mmoja wao kafia wodini baada ya basi la New Force lilikokuwa linatokea Msamvu kwenda Mikese kugongana na gari dogo la abiria (Hiace) yenye namba za usajili T962 BSE lililokuwa linatokea Msamvu, mkoani Mogororo.
Pia watu kadhaa ambao idadi yao ni:-
Waliokufa – 6
Wanaume -1 dereva wa hiace
Wanawake -5 (wote walikua kwenye hiace) mmoja wao kafia wodini
Majeruhi wako 9.
Wanawake – 3
Wanaume – 6

Mashuhuda wa ajali hiyo wanasema chanzo ni dereva wa gari hilo la Hiace kutaka kulipita gari la mchanga lililokuwa mbele ambapo lilijikuta likigongana uso kwa uso na basi hilo.
