
Mmoja wa wanawake aliyetunukiwa cheti kutoka Vodacom, Happynes Shuma (kulia) kutokana na mchango wake wa kuhamasisha, kujitambua kwa wanawake na kutoa mchango chanya wa kuleta mabadiliko katika jamii ya wanawake.


Mkuu wa Maduka ya rejareja kotoka Vodacom, Prigita Steven (kushoto) akikabidhiwa cheti kutokana na mchango wake kwa jamii.




Hafla hiyo ikiendelea.
MTANDAO wa simu za mkononi wa Vodacom Tanzania, leo umezindua rasmi maadhimisho ya Siku ya Wanawake Duniani kwa hafla fupi iliyofanyika makao makuu ya mtandao huo yaliyopo Victoria jijini Dar es Salaam na kuhudhuriwa na wafanyakazi wa vitengo mbalimbali wa mtandao huo.
Lengo kuu la maadhimisho hayo ni kumwezesha mwanamke kujikwamua na kutumia fursa zilizopo kufikia malengo yake kimaendeleo.
Pia mtandao huo umewatambua na kuwatunuku vyeti mabingwa wawili wanawake wanaohamasisha kujitambua kwa wanawake na kutoa mchango chanya wa kuleta mabadiliko katika jamii ya wanawake.