The House of Favourite Newspapers

Lynn: Siolewi Bongo, Wanaume Wababaishaji

Irene Hillary ‘Lynn’

VIDEO Queen ambaye alishawahi kukwaa skendo ya kutoka kimapenzi na mwanamuziki maarufu, Nasibu Abdul ‘Diamond’, Irene Hillary ‘Lynn’ amefunguka kuwa kamwe hatarajii kuolewa na mwanaume Mbongo kwa sababu wengi ni wababaishaji.

 

Akizungumza na Risasi Jumamosi, Lynn alisema kuwa ameona wanaume wengi wa Kibongowanapenda sana kuchezea wanawake hivyo haoni sababu ya kuutesa moyo wake kwa kuwa na uhusiano wa kimapenzi na Mbongo.

 

“Yaani kwa niliyoyapitia sitarajii kabisa kuolewa na Mbongo wala sina wazo hilo kabisa maana naona wazi nitautesa moyo wangu bure,” alisema Lynn ambaye aliuza sura kwenye video ya wimbo wa Kwetu wa Rayvanny.

Stori: Imelda Mtema.

Comments are closed.