Real Madrid Wao Ni Mbappe Tu
JINA la Kylian Mbappe linaendelea kutajwa kuwa mmoja wa wachezaji wanaow aniwa kwa ukaribu na wababe wa Ulaya, Real Madrid licha ya mchezaji huyo kusisitiza kuwa hana mpango wa kuhama kutoka Paris Saint-Germain (PSG) kwa sasa.
Mbappe alionyesha kiwango cha juu akiwa na Ufaransa katika Kombe la Dunia na kuiwezesha timu hiyo kubeba ubingwa, amekuwa akipigiwa debe kwa kiasi kikubwa k u s a j i l i w a na kuonekana anafaa kuibeba Madrid baada ya kuondoka kwa Ronaldo.
Tangu Kuondoka kwa Cristiano Ronaldo kwenda Juventus, Madrid au Los Blancos wamekuwa wakipambana sokoni kuhakikisha wanafanya usajili wa staa mkubwa kama ilivyo kawaida yao kwa ajili ya kuziba pengo hilo.
Taarifa za ndani ya Madrid zinaeleza kuwa Mbappe ambaye ana umri wa miaka 19 bado anaonekana kuwa ni chaguo sahihi na ndiyo maana mabosi wanahaha kuhakikisha wanalifanikisha hilo.
Sifa zimekuwa nyingi ambazo zinambeba chipukizi huyo kusajiliwa ikiwemo kuonyesha makali akiwa na umri mdogo kuanzia ngazi ya klabu hadi timu ya taifa.
Kingine ni uwezo wake wa kufunga, amekuwa akionyesha makali katika ufungaji licha ya kuwa siyo straika halisi, kazi yake imekuwa nzuri licha ya kuwa amekuwa katika kikosi kimoja na mastraika halisi wenye uwezo wa juu.
Hiyo inanogesha kwa kuwa inaonekana kama anafuata nyayo za Ronaldo ambaye naye alikuwa winga lakini mwenye uwezo mkubwa wa kufunga.
Kibiashara pia nyota huyo anaonekana kuwa vizuri kwa kuwa hadi sasa sura yake imekuwa na soko kubwa PSG, hivyo upande mwingine Madrid wanaamini biashara itakuwepo wakimsajili.
Comments are closed.