×

WAVUVI KUNDUCHI WAOMBA KUUZIA SAMAKI SOKO LA FERI

Mkurugenzi wa Kampuni ya Laxspacer International Ltd katika Wilaya ya Kinondoni, Kasmiry Mwabena,  akizungumza na wavuvi wa eneo la Kunduchi jijini Dar es Salaam.
Mmoja wa viongozi wa wavuvi, Faki Mbaruku (kulia),  akitoa mrejesho walioupata kutoka kwa Mkurugenzi wa Wilaya ya Kinondoni.
Baadhi ya wavuvi wawakisikiliza viongozi wao.

WAVUVI wanaofanya shughuli zao katika eneo wa Kunduchi jijini Dar es Salaam, wameiomba Manispaa ya Kinondoni kuwaruhusu kwenda kufanyia biashara zao za kuuza samaki katika soko la Feri kwani eneo lao hapana wanunuzi na wanakuwa na samaki wengi.

 

Hayo waliyasema wakati walipokuwa wakizungumza na Mkurugenzi wa Kampuni ya Laxspacer International Ltd, Kasmiry Mwabena,   ambao ni  wakusanyaji  wa kodi za serikali ambapo aliwataka wavuvi hao kuchukua risiti pale wanapokuwa wamelipia kodi ili kurahisisha kutodaiwa tena wanapohitaji kwenda wilaya nyingine kuuza samaki hasa soko la Feri la Wilaya ya Ilala kwani lipo ndani ya mkoa mmoja.

 

Mwabena alisema kwamba tayari kuna  baadhi ya viongozi  wa upande wa wavuvi ambao wamekwenda kwa mkurugenzi wa wilaya ya Kindondoni na  wamepanga kuangalia namna ya wavuvi hao watakavyoweza kutoa samaki sehemu moja kwenda nyingine kadiri watakavyoona.