The House of Favourite Newspapers

MWILI WA SAJENTI UNARUHUSU VIZAZI VYA MITEGO

Husna Iddy ‘Sajent’

MSANII wa filamu Bongo, Husna Iddy ‘Sajent’ amesema kuwa hata kama akivaa vivazi vya mitego haisumbui kwa mtu yeyote kwa sababu mwili wake unamruhusu kufanya hivyo na ndio maana hafikirii mara mbili anapoamua kuzivaa.

Akizungumza na Ijumaa, Sajenti alisema kuwa watu wengi kwenye mtandao walikuwa wakimnanga kwa kuvaa mavazi ya kujiachia mwili lakini ni kwa sababau anajiamiani na sio kwamba ana kasoro yoyote kwenye mwili au makovu yanayomfanya avae nguo fupi za kumfunika miguu.

“Sinaga kujibana kwenye mwili lakini pia wanaosema navaa nguo fupi sana ndivyo nilivyozoea kwa sababu sina tatizo lolote kwenye mwili wangu wala kovu hivyo nguo kama hizo ni kama zote na siwezi kuacha hata siku moja,” alisema Sajenti.

STORI: Imelda Mtema

Comments are closed.