
TAMASHA kubwa la mkesha wa kufunga mwaka 2018 na kuukaribisha 2019 linatarajiwa kufanyika Desemba 31 Uwanja wa Taifa jijini Dar es Salaam.
Mkesha huo utakaokuwa wa aina yake, unatarajiwa kumdondosha mwanamuziki wa nyimbo za Injili kutoka nchini Nigeria anayejulikana kwa jina la Chris Shalom, anayetamba na wimbo wake maarufu uitwao ‘My Beautifier’ na nyingine nyingi.
Pamoja na Chris Shalom pia waimbaji wengine mbalimbali mahiri kutoka hapa nchini akiwemo Jesica Honore, Goodluck Gosbert, Joel Lwaga na John Lisu wanatarajiwa kutumbuiza.
Mkesha wa mwaka 2019 umeandaliwa na Nabii (Prophet) Clear Malisa wa Passion Java Ministry, kutoka Ubungo-Kibangu jijini Dar es Salaam. Waigizaji/wachekeshaji na watu maarufu mbalimbali kutoka ndani na nje ya Tanzania wanatarajiwa pia kuwepo, akiwemo Pastor Kuria kutoka Show ya Churchchill nchini Kenya.
Katika tamasha hilo hakuna kiingilio na usafiri utatolewa kwa watu wote katika vituo vyote vikubwa vya usafiri Dar es Salaam. Mkesha wa mwaka 2019, umedhaminiwa na Clouds Media Group, Elishadai Shopping Center na Fair Travel Adventures