
SHOO kubwa ya aina yake ya kuufungua mwaka 2019 iliyopewa jina la Masauti Luxury itakafanyika leo katika Viwanja vya Life Club Mwenge jijini Dar es Salaam.
Wasanii watakaofanya shoo ni mwanadada ‘lejendari’ kwenye muziki wa Bongo Fleva, Judith Wambura ‘Lady Jay Dee’, mkongwe wa muziki wa dansi, Christian Bella ‘Obama,’ Aslay Isihaka, Hellen George ‘Ruby’ na Beka.
Kiingilio ni 30,000/= kawaida, 50,000/- VIP na meza ya watu 7-8 500,000/- ikiwa na Bucket ya Jackdaniel yenye full package ya 200,000/=.
