KIKOSI cha Simba Queens kimefanikiwa kuibuka na ushindi wa mabao 7-0 dhidi ya Yanga Pricness katika mchezo wa Ligi ya Wanawake Tanzania maarufu kama Serengeti Women’s Premier League uliochezwa Uwanja wa Karume.
Mchezo huo ambao ulikuwa ni wa ushindani mkubwa na ni kwa mara yya kwanza wanakutana kwenye mchezo huu kutokana na Yanga Princess kupanda msimu huu.
Mabao ya Simba Queens yalifungwa Amina Ramadhani bao 1, Mwanahamis Omari mabao 4, Frola Kayanda mabao alijifunga 1 na Amina Ally 1.

