Mwanamuziki wa Hip Hop Bongo ambaye pia ni Mbunge wa Mikumi kwa tiketi ya Chadema, Joseph Haule ‘Profesa Jay, amesimama Bungeni katika kipindi cha Maswali na majibu na kuuliza kuhusiana na ukarabati wa barabara ya Dodoma Morogoro ambayo ilipata tatizo maeneo ya Dumila.