SPIKA wa Bunge Job Ndugai amesema ipo haja ya kusimamisha Mshahara na Malipo yote ya Mbunge wa Singida Mashariki Tundu Lissu kutokana ana Ofisi yake kutokuwa na Taarifa sahihi ya mahali alipo kwasasa na anachokifanya huko.
Spika Ndugai ametoa taarifa hiyo leo Alhamisi, Februari 7, 2019 Bungeni jijini Dodoma wakati akijibu Muongozo wa Mbunge wa Geita, Joseph Kasheku ‘Msukuma’ ambapo amesema Mbunge huyo hayupo Hosipitali,Hayupo Bungeni na hayupo Tanzania wala hajulikani anafanya kitu gani huko aliko hivyo hana sababu ya kuendelea kulipwa.
Comments are closed.