
Msanii wa muziki kutoka lebo ya Wasafi Classic Baby (WCB), Mbosso, alipiga shoo yaaina yake usiku wa utoaji wa Tuzo za Sinema Zetu International Film Festival, (SZIFF 2019) zilizofanyika Jumamosi iliyopita, Februari 23, katika ukumbi wa Mlimani City, Dar es Salaam.

Mgeni rasmi alikuwa Naibu Spika wa Bunge, Dkt. Tulia Ackson, akiambatana na Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, Dkt. Harrison Mwakyembe, Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Paul Makonda na Mkuu wa Wilaya ya Kisarawe, Jokate Mwegelo.



PICHA NA RICHARD BUKOS | GPL