
KAIMU Mwenyekiti wa Klabu ya Yanga ya jijini Dar es Salaam, Samuel Lukumay, na Mwenyekiti wa Kamati ya Usajili, Hussein Nyika, wametangaza kujiuzulu nafasi zao.
Wawili hao wameamua kuachia ngazi mapema ili kupisha mchakato wa uchaguzi mkuu wa klabu ambao utakaofanyika hivi karibuni.
Pamojana kujiuzulu, Nyika amewaomba msamaha wote aliowakosea pindi akiwa madarakani katika klabu hiyo.
”Ninajiuzulu nafasi zangu zote nikiwa mjumbe wa kamati ya utendaji. Lakini pia nikiwa mwenyekiti wa kamati ya usajili na kamati ya mashindano, na niombe msamaha kwa wale niliowakosea katika utekelezaji wangu wa majukumu,” alisema’.
Hivi karibuni Mwenyekiti wa Bodi ya Wadhamini wa Yanga, George Mkuchika, alitangaza kuwa watakuwa na mkutano mkuu maalum utakaoamua kama klabu inahitaji kufanya uchaguzi mkuu ama la wa kujaza nafasi zilizo wazi.
Mkutano huo unatarajiwa kufanyika siku za usoni ili kufikia mwafaka ili kufanya uchaguzi mkuu mwaka huu ili kutoingiliana mwakani na uchaguzi mkuu wa rais, wabunge na madiwani nchini.