The House of Favourite Newspapers

Yanga Yaanza na Tshishimbi

MSIMU ujao kweli utakuwa moto sana kwani Yanga tayari imeshampa mkataba wa miaka mawili kiungo, Papy Kabamba Tshishimbi. Tshishimbi ambaye alijiunga na Yanga misimu mawili iliyopita akitokea Klabu ya Mbabane Swallows ya nchini Eswatin.

 

Mara kadhaa Tshishimbi baada ya mkataba wake kuelekea ukingoni alikuwa
akihusishwa kutua Azam na Simba kutokana na Yanga kushuka kiuchumi na kusababisha wachezaji washindwe kupata mishahara yao kwa wakati.

 

Akizungumza na Championi Jumamosi, Makamu Mwenyekiti wa Yanga, Frederick Mwakalebela alithibitisha Yanga yaanza na Tshishimbi Dar Wilbert Molandi, Dar es Salaam jana jioni kuwa, Tshishimbi amesaini mkataba mwingine wa miaka miwili ya kuendelea kubaki Jangwani.

 

“Tshishimbi tumemuongeza mkataba wa miaka miwili kwani alikuwa sehemu ya mapendekezo ya kocha wetu, Mwinyi Zahera ambayo aliyatoa tangu mapema,” alisema Mwakalebela.Sweetbert Lukonge, Dar es Salaam

HAJI MANARA Atoa Taarifa SIMBA Watakavyopokea Kombe kwa Msafara

Comments are closed.