The House of Favourite Newspapers

RIHANNA ASHTAKIWAA NA MWENYE ULEMAVU WA MACHO

Related image

MWANAMUZIKI Rihanna a.k.a Badgalriri amelalamikiwa na mwanamke mmoja mlemavu wa macho aliyefahamika kwa jina la Beatriz Gutierrez kwa madai kuwa tovuti ya  bidhaa za Fenty.com hawajatoa nafasi kwa watu wenye ulemavu wa macho kuweza kupata huduma ya kununua bidhaa mtandaoni.

Hii iliwahi kumtokea Beyonce pia ambapo shabiki mmoja mlemavu wa macho alimshtaki kwa kutoweka hitaji hilo kwenye tovuti yake siku chache baada ya kuziweka picha zake za show ya Coachella 2018.

Tovuti ya The Blast limeeleza namna nyingi za kumfanya mlemavu wa macho kuweza kununua bidhaa mtandaoni ikiwemo kusomewa au aina ya maandishi ambayo yanawezesha usomaji.

 

 

Comments are closed.