
MWANAMUZIKI wa Nyimbo za Injili Christina Shusho leo Alhamisi 18, 2019 amefika Ofisi za Global Group kufanya mahojiano katika kipindi Cha ‘Round About’ kinachoruka kupitia Global TV kila Jumapili.
Mtangazaji wa kipindi hicho Calvin Nyorobi akiongea na Mtandao huu wa Global Publishers amesema kuwa christina shusho amefunguka mambo mengi hususani yanayohusiana na huduma yake iliyopelekea kupata tuzo kumi na tatu kutoka Tanzania na nje ya Tanzania.
Aidha Nyorobi ametanabaisha kuwa Christina amegusia kuhusu Rose Muhando pamoja na Marehemu Ruge Mutahaba.
Usikose kutazama kipindi hicho siku ya Jumapili saa 11 jioni kupiti Global tv Online.
Subscribe hapa => GLOBAL TV ONLINE




