The House of Favourite Newspapers

Wanafunzi 13 Chuo Kikuu Wauawa

Watu 13 wamefariki dunia kufuatia vurugu za mapigano zilizotokea katika Chuo Kikuu cha Kogi katika eneo la Ayingba nchini Nigeria.

 

Kwa mujibu wa habari kutoka katika vyanzo vya nchi hio, mapigano hayo yalitokea baina ya makundi mawili ya wanafunzi, kutokana na vurugu hizo za mapigano zaidi ya wanafunzi 13 wamefariki dunia huku wengi zaidi wakiwa wamejeruhiwa.

 

Msemaji wa polisi katika jimbo la Kogi, Hakeem Busari alitoa taarifa kwamba timu za usalama zimetumwa katika eneo hilo, na kwamba uchunguzi kuhusiana na na tukio hilo umeanza.

Comments are closed.