
Mtendaji Mkuu wa Klabu ya Simba, Senzo Mazingisa ambaye ni raia wa Afrika Kusini leo, Alhamisi, Novemba 14, 2019, amefanya ziara ya kikazi katika ofisi za Kampuni ya Global Publisher inayochapisha magazeti bora nchini ya michezo ya Championi na Spoti Xtra.

Mbali ya magazeti hayo ya mengine ambayo siyo ya michezo ni Ijumaa, Ijumaa Wikienda, Risasi, Amani na Uwazi.

Akizungumza katika ziara hiyo, Senzo amesema amepania kufanya makubwa ili kuipa Simba Sc mafanikio makubwa ya Kisoka Afrika na duniani.

Katika ziara hiyo, Mazingisa akiwa na Mjumbe wa Kamati ya Utendaji ya Simba, Mulamu Ng’ambi walitembelea vitengo mbalimbali pamoja na kujionea shughuli za uzalishaji wa magazeti.

Lakini pia alitembelea katika studio ya Global TV Online pamoja na studio za +255 Global Radio kutazama namna ambavyo habari zinachakatwa na vituo hivyo kisha kurushwa kwa jamii.

Kujua zaidi mambo mengi aliyozungumza Senzo, nunua Gazeti la Championi kesho Ijumaa, Novemba 15, 2019.

Senzo akizungumza na Saleh.

Senzo kwenye picha ya pamoja na Wahariri wa Championi, Kitula wa kwanza kushoto, Nkini wa pili kushoto, Waandishi Ibrahim Mussa na Martha Mboma.

Senzo na waandishi wa Championi na Spoti Xtra.

Senzo akielezwa jambo na kiongozi wa Global TV Online, Abdallah Ng’azi, mwenye miwani.

Senzo akiwa nje ya studio za +255 Global Radio.

Senzo ndani ya studio za +255 Global Radio.

Senzo akiwa na Mkurugenzi wa Global Group, Eric Shigongo, ofisini kwake.

Senzo na Ng’ambi akiagana na Saleh.
PICHA NA MUSA MATEJA | GPL