
TAASISI ya Repoa na Wizara ya Nishati na Madini kwa kushirikiana na Ubalozi wa Norway jana wamezindua kitabu kinachohusu utafiti wa nishati hizo.

Kitabu hicho kinaelezea jinsi utafiti wa nishati hiyo ilivyofanyika hapa nchini huko Songosongo na Mnazi Bay na kujadili mambo mbalimbali ikiwemo faida ya nishati hizo itakavyoinua uchumi wa nchi.

Akiongea katika uzinduzi huo uliofanyika Hyatt Regency Kilimanjaro Hotel, Dar, Kamishna Msaidizi wa Gesi wa Wizara ya Nishati, Sebastian Shana, amesema gesi hiyo itasaidia maendeleo ya taifa ambapo mpaka sasa asilimia 54 ya gesi imeshaanza kutumiwa na shirika la umeme nchini (Tanesco).

Shana amesema pamoja kutumiwa na Tanesco, itatumika pia kwa matumizi mengine ambapo tayari kuna magari 300 hapa nchini ambayo yameanza kutumia gesi hiyo.

Katika uzinduzi huo wadau mbalimbali waliohudhuria waliupongeza utafiti uliofanywa kwenye kitabu hicho ambacho kitapatikana sehemu mbalimbali ikiwemo mtandaoni.


HABARI/PICHA: RICHARD BUKOS /GPL