×

Hudefo Yaendesha Mdahalo wa Nishati Jadidifu

Mwanzilishi wa HUDEFO, Sara Pima,  akifungua kongamano hilo.

 

ASASI isiyo ya kiserikali ya Human Dignity and Environmental Care Foundation (HUDEFO) inayojihusisha na utu na mazingira jana iliandaa mdahalo uliohusu utunzaji wa mazingira yakiwemo matumizi ya nishati jadidifu.

 

Baadhi ya viongozi wa serikali za mitaa wakifuatilia mdahalo huo.

 

Mdahalo huo ulizihusisha taasisi za kiserikali, likiwemo shirika la ugavi wa umeme nchini (Tanesco), wakufunzi na wanafunzi kutoka Chuo Kikuu cha Dar es Salaam, Chuo Kikuu cha Dodoma (Udom) na vyuo vingine. Pia kulikuwa na taasisi zingine za dini, benki na nyinginezo.

 

Sehemu ya wadau wakifuatilia mdahalo huo.

 

Mdahalo huo pia ulihudhuriwa na viongozi wa serikali za mitaa ambao ni wadau wakubwa wa mazingira katika jamii.

 

Mmoja wataalamu wa mazingira akitoa elimu kwenye mdahalo huo.

 

Katika mjadala huo mambo mbalimbali yalijadiliwa kuhusiana na matumizi bora ya nishati jadidifu na  madhara ya kutumia nishati zinazosababisha uharibifu wa mazingira.

 

Mhandisi Mkuu Utafiti kutoka Tanesco makao makuu, Samwel Lukas,  akichangia mada kwenye mdahalo huo.

 

Imeelezwa katika kongamano hilo kuwa baadhi ya nishati zinazosababisha uharibifu wa mazingira ni pamoja na kuni na mkaa.

 

Mdau wa mazingira, Madam Violeth,   akielezea uzoefu wake kuhusiana na mazingira.

 

Ilifahamika pia kuwa kwa mwaka watu zaidi ya 22,000 ulimwenguni wanapoteza maisha kwa kuvuta moshi  kutokanana kutumia kuni.

 

Mjadala ukiendelea.

 

Akizungumza kwenye mdahalo huo muanzilishi wa HUDEFO, Sara Pima,  amesema tatizo kubwa na uharibifu wa mazingira lipo vijijini ambapo wananchi wengi hawana elimu ya kutosha ya mazingira.

 

Miongoni mwa wadau wakifuatilia mdahalo kiumakini. 

 

Pima amesema katika kuokoa mazingira, HUDEFO itakuwa ikifanya midahalo hiyo kila mwezi ambapo watakuwa wakizunguka sehemu mbalimbali.

 

Bango la HUDEFO.

 

             Mmoja wa washiriki wa mdahalo huo akitoa mchango wake.

HABARI/PICHA: RICHARD BUKOS /GPL

 

Leave a Comment