Rais Magufuli Aprili 16, 2020 kupitia ukurasa wake wa Twitter amesema ‘‘Ndugu zangu Watanzania, kutokana na ugonjwa wa Corona, nawaomba tutumie siku 3 za kuanzia tarehe 16 – 18 Aprili, 2020 {Ijumaa, Jumamosi na Jumapili} kumuomba Mwenyezi Mungu aliye muweza wa yote atuepushe na janga la ugonjwa huu. Tusali kwa kila mmoja kwa imani yake, atatusikia.”
