ALIYEKUWA Rais wa Marekani, Barack Obama, ametangaza kumuunga mkono aliyekuwa makamu wake, Joe Biden, kupeperusha bendera ya chama cha Democratic kumenyana na Rais Donald Trump wakati wa uchaguzi mkuu mwezi Novemba mwaka huu.
Mpinzani mkuu wa Biden, Bernie Sanders, alijondoa katika kinyang’anyiro cha kutafuta bendera ya chama hicho katika dakika za lala-salama.
Hii hiyo inampa nafasi ya moja kwa moja Biden kuchuana dhidi ya Trump anayemaliza muda wake katika uchaguzi wa Novemba mwaka huu.