


Katika kuunga mkono juhudi kubwa zinazofanywa na Serikali katika kujikinga na ugonjwa wa hatari wa Corona (COVID -19) Kampuni ya Vinywaji ya Cocacola_kwanza imekabidhi vifaa saidizi vya kujikinga na ugonjwa kwa Mkuu wa wilaya ya Ilala, Bi Sophia_Mjema na kwa kupitia Kampeni ya kitaifa ya ‘mikonosafitanzaniasalama’ inayoongozwa na Mrisho Mpoto ikiwa ni mchango wao kwa jamii ili kuimarisha na kusaidia jamii iliomstari wa mbele katika kukabiriana na ugonjwa huo na kuleta jamii ilio huru na magonjwa.
Vifaa hivyo ni pamoja na Barakoa, Gloves, Matenki ya kunawa mikono (pasipo kushika vifungulio vya maji na sabuni), pamoja na vinywaji jamii ya cocacola.