
BEKI wa Yanga, Andrew Vincent ‘Dante’, amesema kuwa yupo fiti kwa asilimia zote, lakini anashangaa kwa nini hachezi ndani ya kikosi hicho.
Dante awali alitajwa kujiondoa Yanga kwa madai ya kushinikiza malipo ya fedha zake za usajili, lakini alirejea kikosini baada ya jambo lake kuwekwa sawa na Shirikisho la Soka Tanzania (TFF).
Akizungumza na Championi Ijumaa, Dante alisema amekuwa akijitahidi kuonyesha uwezo wake na kujituma mazoezini, lakini hapati nafasi.
“Tangu nimerejea kwenye kikosi nimekuwa nikijituma kufanya mazoezi ya pamoja na wenzangu, hivyo naamini kwa kiasi kikubwa niko fiti kwa ajili ya kupambana kwenye mchezo wowote.
“Lakini kwa bahati mbaya nimekuwa sipati nafasi ya kutosha na kiukweli kama utaniuliza ni kwa nini hali hiyo inatokea basi nitakujibu sijui,” alisema Dante.
Stori na Joel thomas,dar es Salaam