
MFUNGWA ambaye alihusika na kumpiga gerezani msanii wa miondoko ya Rnb R. Kelly ,amehukumiwa kifungo cha maisha baada ya kukutwa na hatia kwa kosa la kushambulia mfungwa mwenzeke gerezani.
Muhuni huyo anaefahamika kwa Jina la Jeremiah Farmer, amekutwa na hatia hiyo katika mahakama ya Hammond Indiana, huko nchini Marekani.
Oktoba Mwaka Jana, Wakili wa R.kelly aliwasilisha kesi ya Mteja wake kushambuliwa na Wahuni katika Gereza ambalo amefungwa , na kuomba Mahakama iwachukulie hatua waliohusika au imuachie kwa dhamana R.Kelly Kwa ajili ya usalama wake.