
Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Kassim Majaliwa leo Ijumaa, Januari 22, 2021, amekutana na binti, Miriam Shemndolwa, mkazi wa Mombo, wilaya ya Korogwe mkoani Tanga, ambaye ni mlemavu wa viungo, aliyemuona kupitia televisheni ya TBC.
Waziri Mkuu amemkabidhi binti Miriam hati ya nyumba yake aliyoagiza ajengewe ili iweze kumsaidia katika maisha yake.