
Rais Dk John Magufuli amewataka watanzania kutokuwa na hofu na ugonjwa wa corona na badala yake wanatakiwa kumtanguliza Mungu mbele na kuchukua tahadhari zote za afya.
Dk Magufuli amebainisha hayo leo Februari 21, 2021 aliposhiriki Ibada ya Dominika ya Kwanza ya Kwaresima katika Kanisa Katoliki Parokia ya Mtakatifu Petro Osterbay Jijini Dar es Salaam.
“Tuchukue tahadhari za afya kama zinavyotangazwa inatakiwa kumtanguliza Mungu lakini pia tutafute mbadala wa kupambana na ugonjwa huu ikiwa ni pamoja na kujifukiza, wapo wasaidizi wangu,watoto wangu na wapo wadogo zangu wameshaugua na wamepona” amesema Dk Magufuli.
