The House of Favourite Newspapers

Aliyemzimisha Manula Afunguka Kilichotokea

0

BAADA ya kipa wa Simba Aishi Manula kutolewa uwanjani na kukimbizwa na hospitali baada ya kupata majeraha hatimaye aliyesabisha tukio hilo, Daniel Lyanga ameweka wazi kilichotokea.

Lyanga ambaye ni mchezaji wa zamani wa Simba alisema kuwa haikuwa dhamira yake kumchezea vibaya Manula, badala yake ilikuwa ni ajali ya kawaida mchezoni na hakujua kama Manula yupo nyuma yake wakati anakwenda kucheza krosi ya Kigi Makasi.

Akizungumza na Championi Jumatano, Lyanga alisema Manula alitokea nyuma yake, hivyo hakuweza kumuona na hata yeye alikuja kujua kuwa aligongana na kipa ikiwa yupo chini akiugulia maumivu na akisisitiza kwamba hakufanya makusudi.

 

“Ilikuwa ajali na wala siyo dhamira yangu kumuumiza Manula, unajua yule alitokea nyuma yangu na mimi nilikua naenda kucheza krosi nikashangaa nimegongana na mtu.

Nilikuja kujua kuwa ni Manula baadae baada ya mimi kujisikia vizuri, kwani nilipata maumivu makali,” alisema Lyanga.

 

Manula ilibidi akimbizwe hospitali haraka na kwa mujibu wa kocha Didier Gomes alisema ripoti ya madaktari ilionyesha kuwa anaendelea vizuri baada ya kupata jeraha kichwani.

Stori na Issa Liponda, Dar es Salaam

Leave A Reply