The House of Favourite Newspapers

Hiki Kinampa Jeuri Gomes Kwa As Vita

0

WAKATI Aprili 3, Simba wakitarajia kuvaana na AS Vita ya DR Congo, Kocha Mkuu wa Simba, Mfaransa Didier Gomes amebainisha kitu ambacho kinampa jeuri ya kujiamini mbele ya wapinzani wake hao.

 

Mfaransa huyo ameongeza kwamba kuchukulia siriazi na kujiamini katika mechi zao ndiyo kitu ambacho kimekuwa kikiwabeba na kuifanya timu hiyo kutopoteza mechi yoyote hadi sasa katika Ligi ya Mabingwa Afrika.

 

 

Simba ambao ndiyo vinara wa Kundi A la Ligi ya Mabingwa Afrika watakuwa uwanjani kupambana na Vita katika mechi ambayo Simba wakitoa sare tu watajihakikishia nafasi ya kwenda hatua ya robo fainali, lakini Vita wanahitaji ushindi tu ili wafufue matumaini yao ya kutinga robo fainali.

 

 

Mfaransa huyo amesema kwamba kila mechi ambayo wamekuwa wakiicheza katika hatua hiyo wamekuwa wakijiamini kwamba wanaweza kupata matokeo na hiyo imekuwa msaada mkubwa kwao.

 

 

“Tuko siriazi kwenye kila mechi ya hatua hii kwa ajili ya kuwa bora zaidi baadaye. Tunajiamini kwenye kila mechi kwamba tuna uwezo wa kufanya vizuri na mara zote imekuwa ikitokea hali hiyo.”

Leave A Reply