
MSHAMBULIAJI wa Klabu ya Simba, John Rafael Bocco ametawazwa rasmi kuwa mfungaji bora wa Ligi Kuu Tanzania Bara (VPL) kwa kufikisha jumla ya mabao 16 kwa msimu unaomalizika leo baada ya kufunga bao la nne la timu hiyo dhidi ya Namungo.
Nyuma yake kuna mshambuliaji mwingine wa Simba, Chriss Mugalu mwenye mabao 15, mshambuliaji wa Azam FC, Prince Dude anashika nafasi ya tatu akiwa na mabao 14 wakati Medie Kagere wa Simba ana mabao 13, ni rasmi sasa, Bocco anachukua kiatu cha dhahabu