×

Breaking: Jambazi Aua Askari Wawili Dar, Naye Auawa

HALI ya taharuki imezuka katika eneo la Barabara ya Ali Hassan Mwinyi (karibu na Ofisi za Ubalozi wa Ufaransa), zilizopo Kinondoni Jijini Dar es Salaam, baada ya watu wanaodhaniwa kuwa ni majambazi kutaka kufanya uhalifu katika eneo hilo hii leo Agosti 25, 2021.

Majambazi hao wamewaua Askari Polisi wawili na kuchukua bunduki mbili huku naye jambazi mmoja akiuawa katika majibizano ya risasi. IGP Simon Sirro amethibitisha kutokea kwa tukio hilo.

 

 

Leave a Comment