The House of Favourite Newspapers

Simba Kutua Zanzibar Januari 4

0

MABINGWA watetezi wa Ligi Kuu Bara, Simba wanatarajia kushuka visiwani hapa Januari 4 kwa ajili ya kuanza kushiriki michuano ya Kombe la Mapinduzi ambalo litaanza kurindima Januari 2 mwakani.

 

Timu hiyo iliyopangwa kundi C la kombe hilo itafika siku hiyo huku Januari 5 watashuka uwanjani kuvaana na Selem View mechi itakayopigwa saa 10:15 jioni.

 

Nusu fainali ya mashindano hayo makongwe visiwani hapa itapigwa Januari 10 huku fainali yake ikita­rajiwa kupigwa Januari 13.

 

MAKUNDI MAPINDUZI CUP

 

KUNDI A

Azam

Namungo

Yosso Boys

Meli 4 City

 

KUNDI B

Yanga

Taifa Jang’ombe

KMKM

 

KUNDI C

Selem View

Simba

Mlandege

…..NA KAZIJA THABIT, ZANZIBAR………

Leave A Reply