The House of Favourite Newspapers

Mbeya City Kamili Kuwakabili Simba

0

BAADA ya Bodi ya Ligi kutangaza mabadiliko ya ratiba kwa baadhi ya michezo ya Ligi Kuu Bara, Wagonga Nyundo wa Jiji la Mbeya, Mbeya City wamesema wapo kamili kuwakabili Simba.


Mchezo huo umepangwa
kuchezwa Januari 17, mwaka huu kwenye Uwanja wa Sokoine jijini hapa
ambapo awali ulikuwa
haukupangiwa tarehe.


Akizungumza na
Spoti Xtra, Kocha wa Mbeya City, Mathias Lule, amesema wamejiandaa vema
kuhakikisha wanafanya
vizuri.


“Tunajua utakuwa
mchezo mgumu, tumejiandaa vizuri kuwakabili Simba na tunawaomba mashabiki wajitokeze kwa wingi kuja kutupa sapoti,” alisema.

STORI: DERICK LWASYE, MBEYA

Leave A Reply