×

Makamu wa Rais wa Zanzibar Afanya Mazungumzo na Uongozi wa Vijana ACT- Taifa

Othman Masoud Othman, Makamu wa kwanza wa Rais wa Serikali ya Mapinduzi Zanzibar

MAKAMU wa Kwanza wa Rais wa Zanzibar ambaye pia ni Makamu M/Kiti wa Chama cha ACT – Wazalendo Zanzibar,  Othman Masoud Othman, leo Mei 24, 2022 amekutana na kufanya mazungumzo na Wajumbe wa Kamati ya Uongozi ya Ngome ya Vijana wa Chama cha ACT-Wazalendo Taifa wakiongozwa na Kaimu Naibu Katibu Mkuu wa chama hicho Zanzibar, Ndugu Salim Bimani.

Mwenyekiti wa ACT- Wazalendo, Zanzibar Othman Masoud Othman akiwa na Uongozi wa Vijana ACT- Taifa

Kikao hicho kilichofanyika katika Ofisi ya Makamu wa Kwanza wa Rais Migombani Mkoa wa Mjini Magharibi Unguja, kilijadili masuala mbalimbali yakiwemo yanayohusu maendeleo ya Vijana.M

Leave a Comment