
WATU 31 wameripotiwa kufariki kutokana na sumu ya pombe katika eneo la magharibi mwa India katika Jimbo la Gujarat.
Zaidi wengine 40 wanatibiwa Hospitalini, wengi wao wanasemekana kuwa katika hali mbaya

Polisi wamekamata watu watano wanaoshukiwa kuhusika na tukio hilo. Gujarat inapiga marufuku unywaji wa pombe, lakini bado uzalishaji haramu wa pombe unaendelea kustawi.
Kwa mujibu wa vyanzo vya Habari vya Serikali, pombe hiyo iliyokuwa ikitumiwa na wahanga hao ilikuwa ikiuzwa kinyume na sheria mkoani umo.