×

Wafanyakazi Sita wa Davido Waachiwa, Wawili Ngoma Bado Mbichi

Wafanyakazi sita wa Nyumbani kwa Davido wameachiwa huru huku wawili wakiendelea kushikiliwa Polisi

JESHI la Polisi nchini Nigeria limewaachilia wafanyakazi sita wa nyumbani kwa msanii maarufu David Adedeji Adeleke ‘Davido’, na kuendelea kuwashikilia wawili.

 

Jeshi la polisi katika jimbo la Lagos limewashikilia wawili kati ya wafanyakazi wanane wa nyumbani kwa mwimbaji Davido walioshikiliwa kuhojiwa kuhusu kifo cha mtoto wake wa miaka mitatu, #Ifeanyi.

 

Mtoto huyo kwa bahati mbaya alizama katika nyumba ya babake katika Kisiwa cha Banana mnamo Jumatatu, Oktoba 31. Jana Jumanne Wafanyakazi wanane wa nyumbani walialikwa kuhojiwa.

 

Akizungumza, msemaji wa amri ya polisi ya jimbo la Lagos, SP Benjamin Hundeyin, alisema kufuatia mahojiano makali, wafanyakazi sita wa nyumbani wameachiliwa huku mpishi na yaya wakishikiliwa.

 

Kumbuka kwamba chanzo kilicho karibu na tukio hilo la kuhuzunisha kilisema kwamba Nanny alikuwa na Ifeanyi na Mpishi akaja kuungana nao. Yaya alisemekana kusogea mbali kidogo ili kupokea simu.

Mtoto wa Staa wa muziki Barani Afrika Davido, ameripotiwa kufariki baada ya kuzama ndani ya bwawa la kuogelea

Aliporudi, hakumpata Ifeanyi na kudhani alikuwa na Mpishi lakini Mpishi alisema alikuwa amemwacha Ifeanyi pamoja naye. Walianza kumtafuta Ifeanyi kote nyumbani kwa karibu dakika 20 hadi mlinzi alipomwona kwenye bwawa.

Hakuna aliyeweza kueleza jinsi mvulana huyo alivyoingia kwenye bwawa. Davido na Chioma walisemekana walirejea kutoka kwa safari yao hadi kwenye habari za kuhuzunisha.

 

“Davido alikimbia. Alivua nguo zake na kutaka kukimbilia barabarani. Alizuiliwa. Yeye na Chioma hawawezi kufarijiwa.”

Leave a Comment