The House of Favourite Newspapers

Elon Musk Amrejesha Donald Trump Twitter Baada Ya Kufungiwa Miezi 22

0
Rais Mstaafu wa Marekani, Donald Trump.
Akaunti ya mtandao wa kijamii wa Twitter ya Rais Mstaafu wa Marekani, Donald Trump imerejea kwenye mtandao huo, zikiwa ni siku chache tangu mmiliki mpya wa Twitter, Elon Musk kuonesha nia ya kuirudisha akaunti hiyo.

 

Akaunti ya Trump ilifungiwa kwa muda wa miezi 22 na uongozi uliopita wa Twitter, kwa madai ya kukiuka sheria na kanuni za mtandao huo kwa kuhamasisha vurugu.



Hata hivyo, siku chache zilizopita, Elon aliwataka watumiaji wa Twitter kutoa maoni yao kama Trump arudishiwe akaunti yake au laa ambapo matokeo ya kura asilimia 51.8 waliafiki suala hilo huku asilimia 48.2 wakitaka Trump asirudishwe.
Mmiliki mpya wa Twitter, Elon Musk

“Watu wameamua. Trump anarudishwa,” aliandika Elon kupitia ukurasa wake wa Twitter kuhusu akaunti ya Trump ambayo ilifungwa baada ya wafuasi wake kulivamia Bunge la Marekani, baada ya matokeo ya uchaguzi kutoka na kuonesha kuwa Joe Bidden ameshinda.

#EXCLUSIVE: ALIKIBA AFUNGUKA KUHUSU DIAMOND KUTOA WIMBO BAADA YAKE – “MI SIKEREKI HATA KIDOGO”

Leave A Reply