×

Mwigizaji Bruce Willis Ana Tatizo la Akili, Familia yake Yatangaza

Mwigizaji Bruce Willis ana shida ya kiakili inayofahamika kama frontotemporal, familia yake imetangaza.

Katika taarifa kwenye mitandao ya kijamii, walisema ni “unafuu wa kupata utambuzi wazi”.

Mwigizaji huyo mwenye umri wa miaka 67 aligunduliwa kuwa na aphasia – ambayo husababisha matatizo ya kuzungumza – katika majira ya joto mwaka jana, lakini hii imeendelea na amepewa uchunguzi maalum zaidi, familia ilisema.

Familia iliendelea kusema shida ya akili ya frontotemporal ndio aina ya kawaida ya matatizo kiakili yanayowaathiri watu walio na umri wa chini ya miaka 60.

“Mpaka sasa hakuna matibabu ya ugonjwa huo, tatizo ambalo tunatumai linaweza kutatuliwa miaka ijayo,” ilisema taarifa hiyo.

Willis alipata umaarufu katika miaka ya1980 na 90 baada ya kuigiza katika filamu maarufu kama vile Die Hard, The Sixth Sense, Armageddon na Pulp Fiction.

Pia ameteuliwa kwa tuzo tano za Golden Globes – akishinda moja kwa Moonlighting – na pia Emmys tatu, ambapo alishinda mbili.

Lakini mwaka jana familia yake ilisema kwamba Willis angeacha uigizaji, kwani hali yake ya afya ilikuwa ikiathiri uwezo wake wa kiakili.

VAIBU la MASHABIKI wa TP MAZEMBE, WAKATA MAUNO AIRPORT WAKIIPOKEA TIMU, WAWAIMBA YANGA…

Leave a Comment