
Mshambuliaji wa Argentina na Inter Miami Lionel Messi ameshinda Tuzo ya Ballon d’Or kwa Wanaume kwa mara ya nane.
Mchezaji huyo mwenye umri wa miaka 36 alitambuliwa katika sherehe hiyo mjini Paris baada ya kuisaidia nchi yake kushinda Kombe la Dunia nchini Qatar mwaka jana.
Kiungo wa kati wa timu ya taifa ya Uingereza na Real Madrid, Jude Bellingham ameshinda Kombe la Kopa kwa mchezaji bora wa dunia mwenye umri wa chini ya miaka 21.
Messi alishinda tuzo yake ya Ballon d’Or iliyoongeza rekodi yake mbele ya mshambuliaji wa Manchester City Erling Haaland.
Fowadi wa Ufaransa Kylian Mbappe – ambaye amekuwa mtu wa pili kufunga hat-trick ya mwisho ya Kombe la Dunia katika kupoteza kwa penalti 4-2 dhidi ya Argentina – alimaliza wa tatu.
“Ni vizuri kuwa hapa kwa mara nyingine tena kufurahia wakati huu,” Messi alisema.”Kuweza kushinda Kombe la Dunia na kufikia ndoto yangu.”
Nyota huyo wa zamani wa Barcelona na Paris St-Germain aliongeza: “Sikuweza kufikiria kuwa na kazi ambayo nimekuwa nayo na kila kitu ambacho nimefanikiwa, bahati ambayo nimepata kuwa sehemu ya timu bora zaidi katika historia.
“Zote [tuzo za Ballon d’Or] ni maalum kwa sababu tofauti.”