
Waziri Mkuu wa Thailand amesema kwamba raia 12 wa nchi hiyo waliokuwa wametekwa na Hamas mjini Gaza wameachiliwa huru.
Amesema maafisa wa ubalozi “wako njiani kuwachukua” lakini hakutaja mateka hao walikuwa wapi.
Inafuata Huduma ya Habari ya Jimbo la Misri iliyosema: “Juhudi kubwa za Misri zilisababisha kuachiliwa kwa raia 12 wa Thailand.”

Hakujakuwa na maoni yoyote kutoka kwa Hamas.
Kuachiliwa huru kwa raia wa Thailand sio sehemu ya makubaliano kati ya Israel na Hamas ambayo yalisimamiwa na Qatar.
Bado tunasubiri kuachiliwa kwa Waisraeli 13.