Staa wa filamu za Kibongo, Shamsa Ford amesema anawahurumia wapenzi wa filamu na tamthiliya ambao bado hawajaangalia Tamthiliya ya Jiya kwani wanakosa uhondo mkubwa.
Kuhusu yeye na Aunt Ezekiel, Shamsa amesema wanafanya kazi vizuri pamoja na kwamba uzoefu wao ni miongoni mwa vitu vingine vinavyoifanya tamthiliya hiyo kuwa bora.