
Waziri wa Habari, Mawasiliano na Teknolojia ya Habari, Jerry William Silaa amewateua Watendaji wa Bodi ya Ithibati ya Wanahabari, kwa mujibu wa Kifungu cha 12 cha Sheria ya Huduma ya Vyombo vya Habari Na. 12 ya Mwaka 2016
Uteuzi wa Watendaji wa Bodi hiyo ni kwa Kipindi cha Miaka 3, chini ya Mwenyekiti Tido Mhando
Bodi ya Ithibati ya Wanahabari imeanzishwa kwa Mujibu wa Kifungu cha 11 cha Sheria ya Huduma ya Vyombo vya Habari Na. 12 ya Mwaka 2016
