
OYA Microfinance imehuzunishwa sana na ripoti za tukio la kusikitisha lililotokea Mlandizi, Kibaha, linalodaiwa kuhusisha wafanyakazi wanne wa kampuni yetu, ambalo limesababisha kupoteza maisha.
Tunatoa rambirambi zetu za dhati kwa familia iliyoathirika na kwa jamii nzima katika kipindi hiki kigumu.
Tunataka kuweka wazi kabisa kuwa OYA haijawahi kuidhinisha, wala haitoi mafunzo kwa wafanyakazi wake kutumia aina yoyote ya nguvu katika rejeshaji wa madeni, Taratibu zetu ni za kisheria na zinazingatia maadili, na tukio hili halionyeshi maadili au taratibu zetu za kawaida za uendeshaji.
OYA inashirikiana kikamilifu na mamlaka katika chunguzi wao, Tutaendelea kuheshimu sheria na kudumisha uwazi katika mchakato huu mzima.
Taratibu zetu za urejeshaji wa madeni zinalenga kuwa za heshima na kufuata sheria, na tunachukua hatua za haraka kupitia upya na kuimarisha michakato yetu ya ndani ili kuhakikisha kuwa tukio kama hili halitokei tena.
Tunaendela kujitolea kwa dhamira yetu ya kusaidia na kuwawezesha watu wenye kipato cha chini, na tutaendelea kufanya kazi ili kudumisha imani ya wateja wetu na jamii tunazozihudumia.