The House of Favourite Newspapers

Sita Wakamatwa Kwa Kuhujumu Miundombinu ya SGR

0

Jeshi la Polisi Mkoa wa Dodoma linawashikilia watuhumiwa wawili, Said Sempinga (39) na Michael Robert (44) wote wakazi wa Kilosa kwa tuhuma za kuhujumu miundombinu ya reli ya mwendokasi ya SGR.

Tukio hilo limetokea Oktoba 03, mwaka huu majira ya saa 05 usiku katika kijiji cha Msagali, Wilaya ya Mpwapwa mkoani humo, ambapo watuhumiwa wanadaiwa kukata na kuiba waya wa shaba (copper wire) kutoka katika madaraja matatu ya reli hiyo.

Sambamba na hilo, Jeshi la Polisi linawashikilia watuhumiwa wanne kwa nyakati tofauti kwa tuhuma za kuharibu na kuiba miundombinu ya Serikali kwa kukata nyaya za shaba katika mradi wa treni ya umeme SGR wilaya ya Bahi.

Leave A Reply