
Makamu Mwenyekiti wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) Bara, Stephen Wasira, amesisitiza kuwa Uchaguzi Mkuu wa mwaka 2025 utafanyika kama ulivyopangwa na Tume ya Taifa ya Uchaguzi (NEC).
Akizungumza Katik Mkutano wa Hadhara, 2025, jijini Mwanza Feb 10 2025 , Wasira alieleza kuwa hoja ya kutaka mabadiliko ya Katiba kabla ya uchaguzi huo imechelewa, hivyo uchaguzi utafanyika kwa mujibu wa ratiba iliyowekwa na hakuna chama kinachoiweza kuzuia uchaguzi kwa kuwa uchaguzi upo kwa mujibu wa sheria
Wasira alitoa wito kwa vyama vya siasa, hususan Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), kushiriki kikamilifu katika uchaguzi huo na kuheshimu maridhiano yaliyopo badala ya kushikilia msimamo wa kutaka mabadiliko ya Katiba kabla ya uchaguzi.

