
Jeshi la Marekani limesema kuwa wanajeshi wote sita waliokuwa ndani ya ndege ya kijeshi ya kujaza mafuta angani walifariki dunia baada ya ndege hiyo kuanguka nchini Iraq siku ya Alhamisi.
Marekani imesema tukio hilo halikusababishwa na mashambulizi ya adui, lakini kundi moja la wanamgambo wanaoungwa mkono na Iran limedai kuhusika na ajali hiyo.
Kwa mujibu wa jeshi la Marekani, ndege hiyo ya kujaza mafuta angani aina ya KC-135 Stratotanker ilianguka wakati wa operesheni za kijeshi katika anga ya magharibi mwa Iraq, na uchunguzi kuhusu chanzo halisi cha ajali hiyo bado unaendelea.