×

Mojtaba Khamenei Atoa Onyo Kwa Marekani Kuhusu Vituo vya Kijeshi Mashariki ya Kati

Kiongozi mkuu wa Iran, Mojtaba Khamenei, amesema mataifa ya Mashariki ya Kati hayatatumika tena kama ngao za kulinda vituo vya kijeshi vya Marekani katika eneo hilo.

Kupitia ujumbe uliorushwa na televisheni ya taifa ya Iran wakati wa maadhimisho ya Eid al-Adha, Khamenei alisema Marekani inaendelea kupoteza ushawishi wake katika ukanda huo huku ikikosa maeneo salama ya kuanzisha au kuendesha mashambulizi ya kijeshi.

Kauli hiyo imekuja wakati Iran na Marekani zikiendelea na mawasiliano yanayolenga kufikia makubaliano ya kumaliza vita vilivyoanza Februari 28 na kusambaa katika maeneo mbalimbali ya Mashariki ya Kati.

Ingawa kusitishwa kwa mapigano kulianza Aprili 8, hali bado inaonekana kuwa tete huku pande zote zikitoa tahadhari za kijeshi.

Jeshi la Walinzi wa Mapinduzi ya Iran (IRGC) lilisema limedungua ndege moja isiyo na rubani ya Marekani pamoja na kufyatua risasi kuelekea ndege nyingine zilizodaiwa kuingia kwenye anga ya Iran.

Aidha, jeshi hilo lilionya kuwa litajibu hatua yoyote ya Marekani itakayokiuka makubaliano ya usitishaji vita.

Kwa upande wake, Jeshi la Marekani kupitia Central Command lilitangaza kuwa lilishambulia maeneo ya makombora kusini mwa Iran pamoja na boti zilizokuwa zikidaiwa kuweka mabomu baharini, licha ya kuwepo kwa makubaliano ya kusitisha mapigano.

Vyombo vya habari vya Iran pia viliripoti milipuko katika mji wa bandari wa Bandar Abbas, ingawa havikueleza chanzo chake rasmi.

Mojtaba Khamenei alichukua nafasi ya baba yake, Ali Khamenei, aliyefariki katika mashambulizi ya mwanzo yaliyoongozwa na Marekani na Israel mnamo Februari 28, hali iliyochochea mashambulizi ya kulipiza kisasi kutoka Tehran katika eneo lote.

CCM na CHADEMA BADO NGOMA NGUMU / MWANASHERIA AFUNGUKA TUME ya KIJINAI/BURIANI MAMA MAGUFULI

Leave a Comment