×

Iran Yaridhia Wakaguzi wa Nyuklia, Makamu wa Rais wa Marekani Afunguka

Makamu wa Rais wa Marekani, JD Vance

Makamu wa Rais wa Marekani, JD Vance, amesema Iran imekubali kuruhusu wakaguzi wa nyuklia kurejea nchini humo, hatua inayotajwa kuwa muhimu kwa juhudi za jumuiya ya kimataifa kudhibiti mpango wa nyuklia wa taifa hilo.

Kwa mujibu wa Vance, mazungumzo kati ya Marekani na Iran yamepiga hatua baada ya duru ya kwanza ya mazungumzo yanayolenga kufikia makubaliano ya kudumu ya kumaliza mivutano na migogoro ya kikanda.

Amesema pia kuwa mazungumzo na Shirika la Kimataifa la Nishati ya Atomiki (International Atomic Energy Agency – IAEA) yanatarajiwa kuanza mapema, ikiwa ni sehemu ya mpango wa kurejesha ufuatiliaji wa shughuli za nyuklia nchini Iran.

Katika mazungumzo hayo, pande zote zimejadili pia masuala nyeti ikiwemo kufunguliwa upya kwa Mlango-Bahari wa Hormuz, pamoja na mipango ya uratibu wa kuepusha migogoro ili kuhakikisha usitishaji wa mapigano katika eneo la Mashariki ya Kati, ikiwemo Lebanon.

Kwa mujibu wa taarifa ya pamoja ya wapatanishi kutoka Qatar na Pakistan, pande za Marekani na Iran zimekubaliana kuweka ramani ya njia ya kufikia makubaliano ya mwisho ndani ya siku 60 zijazo.

Vance amesema mazungumzo hayo yameweka msingi mzuri kuelekea suluhisho la muda mrefu, hasa katika kudhibiti mpango wa nyuklia wa Iran ambao Marekani imekuwa ikiutaja kama suala la usalama wa kimataifa.

Ameongeza kuwa hatua hiyo ni ya muhimu kwa Marekani na dunia kwa ujumla, akisisitiza kuwa lengo kuu ni kuhakikisha mpango wa silaha za nyuklia nchini Iran unadhibitiwa kikamilifu kupitia makubaliano ya kidiplomasia.

”DUNIA ya SASA SIYO MAKOMANDO WANAOVUNJA MATOFALI WATAPIGWA na DRONE” – BABA LEVO AWAVUNJA MBAVU

Leave a Comment