×

Mwili wa Kiongozi Mkuu wa Iran Ulivyowasili Tehran Kabla ya Maziko ya Taifa – Video


Mwili wa Kiongozi Mkuu wa Iran, Ali Khamenei, ulivyofika katika eneo la Grand Mosalla jijini Tehran siku ya leo Ijumaa Julai 3, 2026 ukiwa katika maandalizi ya maziko rasmi ya taifa kufuatia kifo chake kilichoripotiwa kutokea Februaryi 28, 2026 katika mashambulizi ya anga ya Marekani na Israel yaliyochochea mzozo mkubwa Mashariki ya Kati.

Kwa mujibu wa vyombo vya habari vya serikali, mamilioni ya waombolezaji pamoja na viongozi mbalimbali wa mataifa ya kigeni wanatarajiwa kushiriki katika sherehe ya mazishi itakayofanyika Jumamosi.

Picha zilizoonyeshwa zilionesha waombolezaji wakiwa wamebeba jeneza la Khamenei lililofunikwa na bendera ya taifa la Iran likiingizwa katika uwanja wa Grand Mosalla, moja ya maeneo makubwa ya kidini na mikusanyiko nchini humo.

Waombolezaji wengine walionekana wakiwa wamevalia mavazi meusi wakishiriki ibada za maombolezo, huku jeneza likiwekwa mbele ya mapambo ya maua mekundu na mandhari ya mapambo ya kijani na nyeupe.

Maandalizi ya mazishi hayo makubwa yanaendelea huku Iran na Marekani zikiwa katika hali ya usitishaji wa mapigano kufuatia makubaliano ya awali ya kusitisha vita.

Shughuli hizo zinatarajiwa kuvuta kati ya waombolezaji milioni 15 hadi 20, jambo ambalo endapo litathibitika litakuwa mazishi makubwa zaidi ya serikali kuwahi kufanyika nchini Iran.

Msemaji wa Bunge la Iran, Mohammad Bagher Ghalibaf, amewataka wananchi kujitokeza kwa wingi kushiriki katika kile alichokiita “siku muhimu katika historia ya Iran ya Kiislamu.”

Mwili wa Khamenei unatarajiwa kupelekwa katika miji mitakatifu ya Najaf na Karbala, kabla ya kuzikwa rasmi Julai 9, 2026 katika eneo la kaburi la Imam Reza mjini Imam Reza Shrine, ambako ndiko alikozaliwa.

Viongozi kutoka mataifa mbalimbali ikiwemo Pakistan, China, Afghanistan na majirani wa Iran wanatarajiwa kuhudhuria, huku pia maelfu ya waombolezaji wakitarajiwa kumiminika kutoka nchi za jirani.

Leave a Comment