×

Mamilioni Wamiminika Kumuaga Kiongozi Mkuu wa Zamani wa Iran Ali Khamenei

Tehran, Iran – Maelfu kwa maelfu ya waombolezaji wamekusanyika katika mji mkuu wa Iran, Tehran, kwa siku ya pili ya shughuli za kumuaga aliyekuwa Kiongozi Mkuu wa Iran, Ali Khamenei, huku mamlaka zikitarajia zaidi ya watu milioni 10 kushiriki katika mazishi hayo.

Sala maalum ya mazishi ilifanyika Jumapili katika ukumbi wa Grand Mosalla, ikiongozwa na mwanazuoni mashuhuri wa madhehebu ya Shia Ja’far Sobhani.

Mwana wa Khamenei na mrithi wake, Mojtaba Khamenei, ambaye ameripotiwa kujeruhiwa katika shambulio la Februari 28, hakuonekana hadharani kwenye ibada hiyo ya mazishi. Hata hivyo, wana wengine wa marehemu, Masoud Khamenei, Mostafa Khamenei, na Meysam Khamenei, walihudhuria shughuli hizo.

Rais wa Iran Masoud Pezeshkian alishiriki ibada hiyo pamoja na viongozi wengine waandamizi wa serikali, akiwemo Spika wa Bunge na mkuu wa mazungumzo ya Iran Mohammad Bagher Ghalibaf.

Jeneza la Khamenei lililofunikwa kwa bendera ya Iran na kuwekwa kilemba chake cheusi, liliwekwa sambamba na majeneza ya ndugu zake wanne waliouawa katika mashambulizi ya Februari 28, akiwemo mjukuu wake mchanga.

Baada ya ibada hiyo, mwili wa Khamenei unatarajiwa kuhamishwa kutoka Grand Mosalla kwa maandalizi ya maandamano makubwa ya mazishi yatakayofanyika katika mitaa ya Tehran siku ya Jumatatu.

CHIKU wa KOMBOLELA – “NIMEOLEWA MARA MBILI -HAKUNA MWANAMKE ASIYEPENDA STARA -NINA WATOTO 2 wa KIKE”

Leave a Comment